Leo Jumanne 21 Aprili 2015 mida ya saa 8 mchana watu wanne
wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wamekamatwa baada ya kumuibia mzungu ambaye jina
lake halikufahamika mara moja, karibu na benki ya Stanbic Kinondoni jijini Dar
es salaam, watuhumiwa hao walifanikiwa kukimbia lakini walikamatwa mtaa wa
Redcross jijini Dar es salaam.
.
Watuhumiwa hao walikuwa na bunduki mbili, na baada ya tukio
hilo mtu mmoja ambae naye jina halikufahamika mara moja aliamua kuwafuatilia
watu hao nyuma nyuma mpaka hapo redcross kwenye mataa ndio akawaziba njia kwa
sababu kuna askari.
Watuhumiwa hao walizobwa njia wakashuka na bunduki ndipo
askari waliokuwepo eneo hilo wakawaweka chini ya ulinzi. na kuwakamata na
kupelekwa kituo cha polisi…..Watuhumiwa hao walikuwa wanne.
No comments:
Post a Comment