• Instagram
  • Twitter
  • Facebook
  • Google+
  • RSS Feed

Wednesday, January 21, 2015

Nimejikuta napenda sana juisi ya karoti ambayo nakunywa walau mara moja tu  kila siku.Watu wengi hawaipendi wanasema sio tamu lakini inategemea imetengezwaje.Katika utengezwaaji ili uenjoy juice yako lazima iwe haina maji yaliyoongezwa wala sukari.Ni juice tuu ya karoti pekeee.
KWAKUNYWA JUICE YA KAROTI UTAPATA FAIDA ZIFUATAZO.
1.Karoti ina carotine ambayo hukupa uwingi wa vitamins A,B,na E
2.Kwa sababu ya uwingi wa madini juice ya karoti inasaidia sana afya ya macho katika kuona vizuri,uimara wa mifupa,meno na kucha.
3.Pia ngozi nyororo nayenye afya bila kusahau nywele.
4.Juisi ya karoti inasaidia kupunguza uwezokano wa kupata kansa ya ngozi na matiti.

5.Ukosefu wa vitamini A husababisha ngozi kukauka,kucha na nywele kuwa dhaifu sasa juisi ya karoti ina uwingi wa vitamin hivyo jusi hii ndio mpango mzima.
6.Kwa sababu ya uwingi huo wa vitamin A husaidia ini kufanya kazi yake ipasavyo.Na inasemekana ili ipatikane vitamin A ya kutosha kunywa juisi hii kila siku sio ukijisikia.
7.Haina cholestral
8.Madini kibao yanapatikana kwenye karoti  Calcium,Potassium,Copper, Iron, Magnesium, Manganese, Phosphorous
9.Kwa mama anaenyonyesha karoti itamsaidia kupata maziwa yenye afya kwa mtoto.
Hizi ni baadhi zipo kibao,kunywa juisi ya karoti kwa afya yako. 

Tuesday, January 20, 2015


Monday, January 19, 2015

The day that i lost you, is the day i lost a part of me i will never be able to recover. I seem okey to people on the outside, but you know how i'm empty within.. I miss your wisdom, advices, motivation, trust, faith, and top of all the tender love and care that can not be measured by any amount.. You will always be a beautiful soul for the countless lives of people you touched.. I will always be a proud son.. I love you with all my heart and strength my queen mother, always have, and forever will.. In Loving Memory 🙏

Sunday, January 18, 2015

Saturday, January 17, 2015

HATUA ZA KUFUATA KATIKA SIMU YAKO....



Bonyeza     *#06#   kujua Imei za Simu yako,kisha ziingize kama ilivyoelekezwa hapo juu.

Tumia Link hii kuchunguza simu yako
 Bonyezahttp://www.imei.info/

Monday, January 12, 2015

Uhali gani msomaji wangu? Ni matumaini yangu kwamba unaendelea vyema na pilikapilika za maisha!

MAONI YAKO YAKOJE?
Nilipoitambulisha mada hii, niliomba tushirikishane mawazo kwani mimi si mjuaji wa kila kitu. Nikushukuru wewe uliyeshiriki kwa kutoa maoni yako kupitia ujumbe mfupi wa maneno (SMS). Natamani kila ujumbe ulionifikia niuchapishe lakini nafasi inanibana. Zifuatazo ni baadhi ya meseji:

1. UNATAFUTA SABABU YA KUACHANA
Haina haja ya kumwandalia fumanizi mwenzi wako kwani kwa kufanya hivyo ni kujenga chuki baina yako na mpenzi wako labda kama humpendi na unatafuta njia ya kuachana naye unaweza kufanya hivyo ili upate kigezo ila kama unampenda usifanye hivyo. Bad Ksoo, Tandika.

2. NILIZIMIA SAA TATU NILIPOFUMANIA
Unapopanga kufumania inabidi ujiandae kwanza kisaikolojia. Mimi niliwahi kumfuma mpenzi wangu tena akivunja amri ya sita na rafiki yangu kipenzi na nilipanga fumanizi ili kuhakikisha kama ninachoambiwa ni kweli.



Nilikuwa siamini kwa jinsi tulivyokuwa tunaishi akionesha kunipenda sana. Hatimaye fumanizi likafanikiwa, siku hiyo mimi nilishindwa kufanya uamuzi, nilizimia saa tatu, dah! Inauma sana. Willy Mwakasanga, Temeke.

3. NI AIBU KUBWA SANA
Kwanza niseme ni fedheha kubwa kumuandalia mwenzi wako fumanizi. Iweje uandae kwa kuwataarifu hata ambao walikuwa hawajui mchepuko wa mkeo/mumeo? Pia ni aibu kubwa kwa wanao na wataathirika sana kisaikolojia, hata wakiwa shuleni watakosa raha kwa kuchekwa na wenzao.
Nyamong’ang’ana Kekarambwe, Geita.

4. FUMANIZI NDIYO DAWA YA MSALITI
Katika kuandaa fumanizi mimi naona kuna umuhimu ili utakapoona au kugundua utakuwa na ushahidi kwamba uliyenaye si mkweli na hana nia njema na wewe maana moyo wa binadamu hauna macho ila akili ndiyo hukataza na kuchanganua zuri na baya.

Utakapogundua ukweli sidhani kama moyo wako utaendelea kumpenda tena katika siku za uhai wako na ni vizuri kufuatilia nyendo za mtu wako ili ujue kama upo sahihi kumpenda au la! Shaibu, Kigamboni.

5. FUMANIZI NI UDHALILISHAJI
Hakuna umuhimu wa kumwandalia fumanizi mkeo, mumeo au mpenzi wako wakati bado unampenda. Kwa mke au mume mwenye busara hawezi kumdhalilisha mwenzi wake, ni aibu kwako wewe uliyefanya hivyo. Nampenda mpenzi wangu na ikitokea nikahisi kitu kibaya kwake, nitakaa naye na kumwambia.
Josephine Maembe, Tabata Kisiwani, Dar.

HITIMISHO
Hakuna tukio baya kama pale unapogundua mwenzi wako anakusaliti lakini hakuna kitu kibaya zaidi kama kumfumania.

Wataalam wa saikolojia wanashauri kwamba kama hujajiandaa kisaikolojia, hutakiwi kuandaa fumanizi. Kama unao ushahidi wa kutosha na unadhani huwezi kuendelea kuishi naye tena kwa sababu ya tabia zake za usaliti, unaweza kutumia njia za busara kukatisha uhusiano wenu.

Pia kama bado unampenda lakini unajua anakusaliti na ushahidi unao, unaweza kuzungumza naye kwa upole, ukishindwa washirikishe watu anaowaheshimu na kama kweli anakupenda, hataendelea kukusaliti, atabadilisha tabia na kutulia na wewe.

Mwisho kabisa ni kwa wale wasiotosheka na mpenzi mmoja na kuendekeza michepuko. Siku hizi kuna maradhi mengi ukiwemo Ukimwi.

Michepuko siyo ujanja, baki njia kuu na huyo mmoja uliyemchagua na kuwa mwaminifu kwake. Sote tukisimamia uaminifu kwenye mapenzi, hakutakuwa na mafumanizi wala maumivu ya moyo!
 Credit:GPL


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
© ALLSTARTZ.BLOGSPOT.COM 2012 - 2017 | ALL RIGHTS RESERVED | CODE + DESIGN BY: DMZ