Tuesday, January 29, 2013
Sunday, January 27, 2013
Thursday, January 17, 2013
MASHAIRI YA STAMINA ft. FID Q - WAZO LA LEO.
Song:Wazo La Leo
Artist:Stamina Feat Fid Q
Studio:Bongo Records
Producer: P funk Majani
Song Writters:Stamina (verses) & Fid Q (chorus)
Intro...
U know what majani??nice to meet you homie
Its moro town baby,,,shorobwenzi
Verse 1. (Stamina)
Elimika nyangema, maisha hayaendeshwi na nguo
Pesa ni vazi la mgema, haliwezi kuwa na mpasuo
Vaa uaminifu,tupa boksi la kondomu
Hip hop haijengwi na bifu,underground usijaze fomu
Maisha ni kujipanga, mganga usigawe irizi
Viongozi msizuie ganja, huku mnachukua ushuru wa rizz
Ridhiki ina kamba, ivute ili ikupe noti
Mkulima rudi shamba,dec mbegu siku hizi hazioti
Maisha njia panda,mtembezi chagua pa kwenda
Uchumi vazi la bwanga,ukishuka uvishe suspenda
Shiba kwa nia,ukiwa mlafi wa malengo
Usikufuru we shukuru ukifaulu kila tendo
Punguza pupa,mpendaji uingie ndoani
Mapenzi yamevaa bukta,uswazi mapaja hadharani
Usilale kijinga,kwenye kitanda cha ushamba
Unaweza kuwa shabiki wa samba,na ukaishi mwembe yanga
Chorus. (Fid Q)
Hiki kijiko unachokiona,baada ya kula kwa mkono
Ndomu usiyoiona,mpaka ukishafanya ngono
Neno la kuponya,lilokosa mdomo
Na hili bonge la ngoma,kwenu kwangu ni kama somo
{Hilo ndo wazo la leo}-inshu usingizi wa furaha,mzinzi jenga kibanda cha angaza utoe nasaha.
{hilo ndo wazo la leo}-usiishi kwa vikwazo,weka wazo kwenye vyanzo vyako-{hilo ndo wazo}
Verse 2.(Stamina)
Underground panga tenzi,ustar hauji kwa promo
Hakuna tajiri wa mapenzi,kapuku punguza ngono
Bora uitwe mfalme jua,kwenye utawala wa kishamba
Mapenzi yakikusumbua,tafuta daktari wa kitanga
Vazi unaloishi,mwenyezi yeye ndio disegner
Shetani akikushawishi, mvute kwake kama dayna
Dunia duara,jitahidi uizunguke
Mla bata starehe hasara,,wekeza hadhi isishuke
Huna undugu na bakhersa,niaje aje unakula unga
Mateja wanahitaji sensa,taifa la kesho linavunda
Dogo jifunze,heshima sio upaparazi
Mwambie na dada ajitunze,mlango wake asiuache wazi
Kama unajijua ni mchoyo,basi usingoje kupewa
Tafuta pesa kwa moyo,sio kwa ushindi wa ngekewa
Sharo mpe salamu,the great braza kanumba
Mwambie bongo sio tamu,na lulu bado wamemfunga
Chorus(fid q)
Hiki kijiko unachokiona,baada ya kula kwa mkono
Ndomu usiyoiona,mpaka ukishafanya ngono
Neno la kuponya,lilokosa mdomo
Na hili bonge la ngoma,kwenu kwangu ni kama somo
{Hilo ndo wazo la leo}-inshu usingizi wa furaha,mzinzi jenga kibanda cha angaza utoe nasaha.
{hilo ndo wazo la leo}-usiishi kwa vikwazo,weka wazo kwenye vyanzo vyako-{hilo ndo wazo}
Verse 3.(Stamina)
Utamu wa ndafu ya harusi,sio wa ndoa we kilaza
Mbuzi atabaki mbuzi,hata mle hadi mkasaza
Nchi tayari imekonda,mwananchi tafuta ulaji
Life ngumu hadi omba omba,kidonda anafanya mtaji
ukipata mazuri,jipange kuikwepa hasara
kijana vazi la msuli,haliwezi kukuvisha busara
ukiishi kwa hisia,kila stone litakubanza
cha msingi ni kuweka nia,ujivue kuwa mtanza
kata ya kijiji,haibebi maji ya maendeleo
katibu tunza mkwiji,msuli ukishuka kimeo
uchumi umeshika tama,kwenye shavu la mlanguzi
raia usilaumu chama,shiriki kwenye uchaguzi
unaweza ukavaa kinga,ila ukafa kwa uaminifu
mzinzi usigawe ujinga,sambaza ujumbe wasifu
hakuna snitch kama pesa,ukiwa nae fanya vya maana
akiondoka atakutesa,utamsaka usiku na mchana
Chorus. (Fid Q)
Hiki kijiko unachokiona,baada ya kula kwa mkono
Ndomu usiyoiona,mpaka ukishafanya ngono
Neno la kuponya,lilokosa mdomo
Na hili bonge la ngoma,kwenu kwangu ni kama somo
{Hilo ndo wazo la leo}-inshu usingizi wa furaha,mzinzi jenga kibanda cha angaza utoe nasaha.
{hilo ndo wazo la leo}-usiishi kwa vikwazo,weka wazo kwenye vyanzo vyako-{hilo ndo wazo}
“Ni kitambo kirefu sana nimekuwa kimya kutokana na maswala ya shule ila
sasa kidogo nimetulia. NImeamua kuuachia wimbo huu unaitwa ROHO MBAYA
ambao nimewashirikisha BELLE 9 na PIPI kama zawadi yangu kwa fans wangu,
lakini official single ya mwaka huu inafuata siku si nyingi. Beat
ilifanywa na Duke wa M-Lab na vocals zilifanywa na Tetemesha Records
mwaka juzi.Tegemeeni mengi mazuri kutoka kwangu kwa mwaka huu – Sajna.
Wednesday, January 16, 2013
Saturday, January 5, 2013
Habari Mabibi na Mabwana!! poleni na mihangaiko ya siku!! naam
ijumaa iliyopita nilitoa
kibao changu maridhawa
kipya kabisa kinaitwa
2030!!!
na nilikiachia kwa
radio stations zote nchini
kadri ya uwezo wangu/wetu, though kutokana na
mawasiliano ni ngumu kufikia radio
zote kwa wakati, ila nyingi
ziliupata!!!
lakini niliweka
utaratibu fulani kwa watakaohitaji kuupata
huo wimbo 2030 mbali na radio basi wataupata kwa
kussuport kuununua on line
kwa tsh 3000/=!!nilishatangaza
sana mnafahamu!!ilikuwa ni trial
ya kuona nani ana love ya kussuport na nani hana kupitia njia zilizowekwa na sio njia nyingine.
zoezi limeenda
kwa challenge nyingi sana asante
wote waliossuport katika
hili, pia asante
kwa wale walioliharibu zoezi hili
maana imenifanya nimtambue
hu z real na hu z fake!!!
imeniuma kuona wapo wasanii wanafanya biashara
kama hii wanauza mix tapes, album,tisherts zikiwa
zote ni movements za kuleta
changes ktk mziki wetu, then hao
hao wanakuwa mstari wa mbele kupinga hii movement yangu halafu bila sababu yani dah SHALL WE MAKE
IT?????
nway lilikuwa ni zoezi
lililopangwa kufanyika kwa week
moja 1 tu ili kuona na kufanya tathmini
kuwa yanawezekana haya?najua wengi wanasubiri feed back ya mauzo haya
haikuwa nzuri sana kwa wingi wa nyomi nililokuwa nalo, lakini
pia haikuwa mbaya maana
ni mageni haya..kwa siku 7 za mauzo
ilikuwa kila siku wananunua watu
wasiopungua 50!! so unaweza
ona hapo kuwa
yanawezekana haya tukiyawekea
mkazo...ILA SIAMINI KAMA KILA MSANII ANAWEZA FANYA, INATEGEMEA NA NGUVU YA MSANII HUSIKA NA KIBAO
ALICHOKITOA..(IFIKIE KIPINDI
TUONGEE UKWELI TUU!!)wengi wameanza kufanya biashara kupitia
nyimbo hii na inawanufaisha wao,
wengi wamerecord radio wimbo huu kitu kilichopelekea kukosa quality na bado wanauzia wengine so wanapewa kitu kisicho na quality,
pia wengi wanakwazika na mengi yaliyoongelewa ndani ya wimbo huu na
wanakosa majibu maana wanakosa fursa ya
kuusikia mara kwa mara kwasababu hawajaunga mkono hii
movement!! au pengine imekuwa ni
njia ngumu kwao kuupata,
basi kwa wale
waliossuport kwa kuinunua nawashukuru sana na mungu awaongezee mlipopungukiwa,
najua litatokea hili la kujiona
wanyonge kuwa ROMA amechukua fedha
zetu na kisha ameachia bure, mi naamini ukiwa muelewa na ukiona
nilichokisema hapo juu hautakwazika as
long umeonyesha lav yako kwa
msanii unayemfeel, samahani sana kama nitakuwa
nimekukosea,nimefanya hivi kama
kuanzisha hiki kitu na naamini
wengine watafatia na
kukiboresha zaidi!!LAZIMA APOTEE
MMOJA ILI KUMI WAISHI VEMA NDIPO YATAPATIKANA MAENDELEO!! AM SO SORRY!!!
So leo wiki imetimia
na wimbo umetoka rasmi na hauuzwi tena
kama ilivyotangazwa awali.
unapatikana bure kwenye
net, download via access yoyote utakayoiona!! nimeutoa rasmi
kwenye blogs mbali mbali
ANZIA NA YA DJ CHOKA, na nyinginezo!!
Na version
iliyopita kuchezwa radio
ni version ya
ROMA ile beat yake iliyochangamka ambayo ni version ya 1 ambayo
ndiyo ilikuwa ya kwanza kutambulishwa ijumaa pale clouds fm radio.
kwa maswali zaidi
tutameet kwenye mainterviewz
huko maradioni na tutawekana sawa!!
samahanini kwa wote
niliowakwaza, asanteni kwa wote
mliossuport!!
Wednesday, January 2, 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)