• Instagram
  • Twitter
  • Facebook
  • Google+
  • RSS Feed

Sunday, February 7, 2016

Samatta Aanza Kwa Kishindo, Timu yake Yashinda 1 – 0

No comments:
 
Baada ya nyota wa Tanzania Mbwana Samatta kufanikiwa kukipiga kwa mara ya kwanza kwenye klabu yake ya KCR Genk, mkali huyo ameandika ujumbe kwenye account yake ya instagram kuwashukuru wale wote wanaom-support na kumtakia mema.
Samatta ameandika ujumbe unaosomeka kama ifuatavyo: “Napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru watanzania pamoja na mashabiki wangu wote wa @krc_genk_ kwa maombi na support yenu, Leo nimefanikiwa kucheza mchezo wa kwanza rasmi nikiwa na klabu yangu mpya @krc_genk_na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa 1-0”.

Kwenye mchezo huo ambao Genk ilikuwa ugenini ikicheza dhidi ya Muscron, Popa aliingia dakika ya 73 kuchukua nafasi ya Nikos Kareli na kumaliza dakika zote zilizo salia.
Mtanzania Mbwana Samatta ameishaanza kuichezea KRC Genk ya Ubelgiji baada ya jana kuingia katika mechi ya ligi na kucheza kwa dakika 17 wakati timu hiyo ilipoivaa Mouscron na kushinda kwa bao 1-0.
Akiwa Ubelgiji, mara nyingi atakuwa akitumia usafiri wa kijamii, yaani treni. Lakini kwa shughuli za timu, Samatta atakuwa akitumia basi la wachezaji.
Samatta anaonyesha ni mtu wa malengo kweli baada ya kuacha magari yake zaidi ya matatu, na kwenda kuanza kutafuta maisha upya Genk.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa TP Mazembe, ameamua kuachana na kila kitu ukiwemo umaarufu wake mkubwa nchini DR Congo na kwenda kuanza upya nchini Ubelgiji kwa kuwa anataka kutimiza ndoto yake.

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
© ALLSTARTZ.BLOGSPOT.COM 2012 - 2017 | ALL RIGHTS RESERVED | CODE + DESIGN BY: DMZ