• Instagram
  • Twitter
  • Facebook
  • Google+
  • RSS Feed

Wednesday, April 27, 2016

Collabo mpya ya Mr.Blue na Alikiba Soon inategemea kutoka

No comments:
 
Nyota wa Bongo Fleva, Herry Samir ‘Mr Blue’ ambaye hivi karibuni aliuaga ukapera kwa kuamua kufunga pingu za maisha na mzazi mwenzake, Wayda, amedai anatarajia kuachia wimbo mpya ambao amemshirikisha Ali Kiba.

Mr Blue amedai kwamba wimbo huo utajulikana kwa jina la ‘Mboga Saba’

Akizungumza na MTANZANIA, Mr Blue alisema kuwa wimbo huo upo tayari na anatarajia kuuachia wiki ijayo endapo mtayarishaji wake, Man Water atamkabidhi.

“Kiukweli huu wimbo haujawahi kutokea na utakuwa bonge la wimbo kwa kuwa tumekutana wakali wa muziki, ninaamini wimbo huo utakuwa ni historia katika tasnia ya muziki hapa nchini,” alisema Mr Blue.

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
© ALLSTARTZ.BLOGSPOT.COM 2012 - 2017 | ALL RIGHTS RESERVED | CODE + DESIGN BY: DMZ