• Instagram
  • Twitter
  • Facebook
  • Google+
  • RSS Feed

Saturday, March 5, 2016

Azam yatoana Jasho na Yanga Taifa, Simba Yachekelea Sare Yao

No comments:
 
IMG_4819

Mchezo wa marudiano wa raundi ya pili wa ligi kuu kati ya Azam FC ambao ndiyo walikuwa wenyeji wa mchezo huo umemalizika kwa timu hizo kutoka sare ya kufungana magoli 2-2 mchezo ambao umechezwakwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.
IMG_5045
Azam walianza kufunga bao la kwanza dakika ya 12 ambalo lilitokana na kujifunga mlinzi wa Yanga Juma Abdul baada ya Kipre Tchetche kupiga shuti ambalo lilipanguliwa na golikipa wa Yanga Ally Mustafa ‘Barthez’ kisha Juma Abdul akajifunga wakati akiwa katika harakati za kuokoa.
Azam-vs-Yanga
Juma Abdul akaisawazishia Yanga bao hilo dakika ya 28 kwa shuti kali ambalo lilijaa moja kwa moja wavuni likimshinda golikipa wa Azam Aishi Manula.
IMG_5030
Yanga wakapata bao la pili mfungaji akiwa ni Donald Ngoma aliyepasia nyavu dakika ya 42 kabla ya John Bocco kusawazisha na kuufanya mchezo huo kumalizika kwa sare ya bao 2-2.
CC
Rekodi za Mechi Zilizopita
Oktoba 17, 2015
Yanga SC 1-1 Azam (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Agosti 22, 2015
Yanga 0-0 Azam FC (Yanga ilishinda kwa penalti 8-7 Ngao ya Jamii)
Julai 29, 2015
Azam 0-0 Yanga SC (Azam ilishinda kwa penalti 5-3 Robo Fainali Kombe la Kagame)
Mei 6, 2015
Azam 2-1 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Desemba 28, 2014
Yanga SC 2-2 Azam (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Septemba 14, 2014
Yanga SC 3-0 Azam FC (Ngao ya Jamii)
Machi 19, 2014;
Yanga SC 1-1 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Septemba 22, 2013;
Azam FC 3-2 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Februari 23, 2013;
Yanga SC 1-0 Azam FC (Ngao ya Jamii)
Novemba 4, 2012;
Azam FC 0-2 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Machi 10, 2012;
Yanga SC 1-3 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
January 07, 2012
Azam FC 3-0 Yanga SC (Robo Fainali Kombe la Mapinduzi)
Septemba 18, 2011;
Azam 1-0 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Machi 30, 2011;
Yanga SC 2-1 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Oktoba 24, 2010;
Azam FC 0-0 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Machi 7, 2010;
Yanga SC 2-1 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Oktoba 17, 2009;
Azam FC 1-1 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Aprili 8, 2009;
Yanga SC 2-3 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Oktoba 15, 2008;
Azam FC 1-3 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
© ALLSTARTZ.BLOGSPOT.COM 2012 - 2017 | ALL RIGHTS RESERVED | CODE + DESIGN BY: DMZ