• Instagram
  • Twitter
  • Facebook
  • Google+
  • RSS Feed

Friday, October 26, 2012

Hali ya afya ya P.Diddy baada ya ajali ya gari yawekwa wazi, nae asema ‘neno’

No comments:
 

Gari ya P-diddy baada ya kupata  ajali

Siku moja baada ya taarifa ya ajali ya gari aliyoipata CEO wa Bad Boy Records maeneo ya Los Angeles kushtua ulimwengu wa burudani, sasa taarifa kuhusu hali yake kiafya imewekwa wazi rasmi na kusambaa kwenye mitandao mbalimbali.

P-diddy akiwa amejilaza kwenye majani baada ya ajali 
Muwakilishi wa rapper huyo mkongwe amesema, “Sean Combs alipata injuries mbalimbali katika ajali ya gari aliyopata jana ikiwa ni pamoja na shingo lake na mbavuni. Sasa hivi anaendelea na matibabu kwa daktari wake kwa ajili ya hizi injuries na angependa kuwashukuru fans wake wote kwa sapoti yao kubwa tangu alipopata ajali.


Jumatano hii police wa Los Angeles wametoa taarifa rasmi na kuthibitisha hilo imesema, “ Sean “Diddy” Combs amepata injuries katika ajali ya gari ambayo ilitokea mbele ya Hotel ya Beverly Hills, na kwamba boss huyo wa Dirty Money na Bad Boy Records alisema atatafuta matibabu yake binafsi.”

Diddy akitoa maelezo kwa polisi waliofika eneo la ajali
Katika ajali hiyo iliyotokea jumatano hii P.Diddy alikuwa anaendeshwa na dereva wake, ambapo gari lake aina ya Cadillac Escalade iligongana na Lexus RX mbele ya hotel ya Beverly Hills na ambulance iliitwa haraka katika eneo la tukio.

Kwa mujibu wa mtandao wa X17 online wahudumu wa hotel hiyo walitoka haraka na kwenda kuwasaidia P.Diddy na dereva wake na alionekana akiwa amejilaza mbele ya garden ya hotel hiyo. Lakini baada ya muda alikataa kupelekwa hospitalini na ambulance na kwamba atatibiwa na mganga wake binafsi.

Mungu ameepusha ajali hii kuwa na madhara makubwa, tumuombee apone haraka aendelee kufanya kazi ya kuwapa shangwe fans kupitia spika kwa hits kibao toka Bad Boys. 

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
© ALLSTARTZ.BLOGSPOT.COM 2012 - 2017 | ALL RIGHTS RESERVED | CODE + DESIGN BY: DMZ