• Instagram
  • Twitter
  • Facebook
  • Google+
  • RSS Feed

Sunday, November 24, 2013

JINSI YA KUONDOA MADOA YA CHUNUSI

No comments:
 



Chukua maji ya rose kiasi kama ni kijiko kimoja na maji ya limao nayo yawe kijiko kimoja paka eneo liloathiriwa na madoa, kaa kwa muda wa nusu saa mpaka saa moja kisha osha uso wako, fanya hivyo kwa muda wa wiki tatu utapona madoa doa yote usoni.
 
Juisi ya limao na liwa
Chukua juisi ya limao kiasi changanya na liwa kisha paka eneo lililoathirika, kaa kwa muda wa dakika tano utaona matokeo. 
Juisi ya limao na unga wa mdalasini pia ni tiba nzuri ya kusafisha uso kuondokana na madoa yote.
 
Asali na mdalasini
Chukua vijiko vitatu vya asali na kimoja cha mdalasini changanya kisha paka usoni pia ni tiba nzuri inasaidia kwa kiasi kikubwa.
Apple na asali
Chukua apple liponde changanya na asali kiasi, kisha paka usoni mbali na kutibu madoa pia inatibu chunusi.
Maji ya kitunguu swaumu
chukua maji ya kitunguu swaumu paka kwenye madoa yote utaona matokeo.
Nyanya 
chukua kipande cha nyanya paka usoni kisha kaa kwa muda wa saa moja nayo ni tiba nzuri.

Tango
Tango pia ni tiba, chukua kipande sugua uso wako kila siku asubuhi utaona matokeo.
Papai 
Chukua papai liponde kisha paka usoni litakusaidia kuondoa tatizo la madoa yote usoni.

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
© ALLSTARTZ.BLOGSPOT.COM 2012 - 2017 | ALL RIGHTS RESERVED | CODE + DESIGN BY: DMZ