• Instagram
  • Twitter
  • Facebook
  • Google+
  • RSS Feed

Saturday, October 27, 2012

No comments:
 

Gari la kusambaza magazeti ya kampuni ya Mwananchi lapata ajali, watu 3 wapoteza maisha, 5

Gari linalosambaza magazeti ya kampuni ya Mwananchi mikoa ya Kilimanjaro na Arusha,limepata ajali wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro na kusababisha vifo vya watu watatu na wengine watano kujeruhiwa.


 Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro Afande Robert Boaz, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo Oktoba 26 majira ya saa 11 alfajiri katika eneo la Kirinjiko, wilayani Same, barabara kuu ya Tanga-Moshi.


 Kamanda alisema Gari hilo lenye namba za usajili T336 BFU Isuzu Pick-up linalosafirisha magazeti ya kampuni ya Mwananchi Communication (MCL)  ililigonga gari lenye namba za usajili T 415 AAM/ T 411AAM Scania na  kusababisha vifo vya watu watatu papohapo.


 Kamanda Boaz amewataja waliofariki kuwa ni Ibrahim Mrutu (65)  mkazi wa wilayani Same, Abdalla Rajabu(49) mkazi wa Majengo Mkoani Arusha ambapo wote ni madereva wa Simba Truck pamoja na Robert Mnyeki (39).


 Aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni Rahim Bakari (28)mkazi wa Kinondoni jijini Dar es Salaam mfanyakazi wa kampuni ya Mwananchi,Juma Said (37)Dereva wa Simba Truck mkazi wa Arusha kwa Mrombo,Gasino Nguma(40) mwalimu mkazi wa Mlandizi jijini Dar es salaam, Hamza Omary (31) mfanyabiashara mkazi wa Buguruni jijini  Dar es salaam pamoja na Sekero Musa (30) ambaye hali yake inaelezewa kuwa mbaya.


 Watu hao walikuwa ni abiria katika gari lililokuwa likisafirisha magazeti ambapo Majeruhi wamelazwa katika Hospitali ya wilaya ya  Same na KCMC kwa ajili ya matibabu.


 Chanzo cha ajali hiyo kamanda alisema ni mwendo kasi wa gari dogo na kwamba dereva wa gari hilo Wambura Ramadhani anashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano na uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo bado unaendelea.

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
© ALLSTARTZ.BLOGSPOT.COM 2012 - 2017 | ALL RIGHTS RESERVED | CODE + DESIGN BY: DMZ